Tangazo Muhimu:

Karibu katika tovuti ya IFM Fellowship CCR,Tafadhali jiskie huru kutoa maoni yako juu ya hii tovuti.

Tuesday, June 21, 2016

HATA UKIWA KWA YESU LAZIMA KUPENDEZA BWANA!!

 Vunja kabati kwa ajili ya Bwana!!!
Na Anamaria Nzamba
Da Tumaini Mfujege somo lako la jumapili iliyopita niliguswa na ule ushuhuda wako hasa pale uliposema, "...baada ya kufunga na kuomba, siku ya kufungua, hali ukijua na ukiamini ulikuwa umefufuka, uliamua kuvaa kifufuko fufuko...." uuuuuuuuuh of coz yes, tena ukatupia kitu cha silver, nguo yako ya kusimamia maids, ukatoka kifufuko... I loved this. ndio maana nimeamua kuandika hapa.
Bwana Yesu nakuhitaji niwezeshe kuandika kwa namna ambayo itakupendeza wewe Zaidi na watu wako kwa ajili ya sifa na utukufu wa jina Lako. Unihurumie eeh Yesu wangu. Ninapenda kukutumikia kwa moyo wangu wote, kwa nguvu zangu zote na kwa uwezo na akili zangu zote. Amen
Kuvaa kifufuko: ukweli kabisa mimi ninaamini katika hili, kama mkristu niliyekombolewa sina budi kuwa na muonekano ambao utanitambulisha katika jamii, kwamba nimefufuliwa, nimekombolewa, Yesu yuko ndani yangu, nami ndani yake, Yesu ananipenda, nami nampenda, ninalindwa, ninamsaada ooh niko na Yesu... etc etc
nikikumbuka hayo yooote, siwezi kuacha kuvunja kabati kila siku iitwayo leo, aliyefufuliwa na Yesu hata kimuonekano tu utamgundua. Anavaa vizuri, anapendeza, na kupendeza haihusiani na gharama kabisa, kuna nguo za kila aina na bei rahisi nzuri ajabu... tupendeze jamani. hebu tuwe tunavunja kabati, maana ukweli kabisa kila siku ni siku mpya na Bwana amejifunua kwetu karibia kila siku. kila mtu anao ushuhuda wa kila siku, sasa kwa nini kama tunafufuliwa kila siku , hatupendezi kila siku...!

Saturday, March 12, 2016

KARIBU SANA NDANI YA FELLOWSHIP YA KARISMATIKI KATOLIKI YA CHUO CHA USIMAMIZI WA FEDHA IFM


Kikundi cha sala cha IFM, kilianzishwa tarehe 25/03/2007 chini ya uongozi wa karismatik katoliki jimbo kuu la Dar es salaam.
Madhumuni ya uanzishwaji ni kuamsha imani za wakatoliki na kanisa kwa ujumla ndani ya chuo cha IFM,vyuo vingine pamoja na parokia ya St Joseph.

Kikundi hiki tangu kimeanzishwa mpaka sasa kinakutana kwa ibada parokiani St. Joseph kila jumapili kuanzia saa tisa na nusu hadi saa kumi na moja na nusu (15:30-17:30) jioni.
Lakini pia kwa kila jumapili ya kwanza ya mwezi huwa tunakutana kwa masaa takriban matatu katika ukumbi mojawapo katikati ya jiji ambapo kwa sasa tumekuwa tukitumia sana HIDERY PLAZA POSTA MPYA.
 Kikundi kilianza na takribani idadi ya watu kumi (10) na imekuwa ikiongezeka kwa kasi siku kwa siku.

karibuni sana tena jumapili hii kwa ajili ya kuendelea na kumsifu , kumwinua MUNGU na kuendelea kujifunza neno lake.

ni pale kanisa la MT YOSEFU katika ukumbi wa wawata ulipo nyuma  ya kanisa mara uingiapo kupitia geti kuu.

kwa mawasiliano zaidi piga namba zifuatazo:
0717 203 772, 0752 507 171, 0656 516 903, 0658 123 232

Sunday, November 17, 2013

SOMO KUHUSU KARISMATIKI KATOLIKI NA HISTORIA YAKE KWA UFUPI

Vipengele vya Somo:

-Utangulizi
-Malengo
-Tunu
-Mafanikio
-Changamoto
-Masuluisho

Charismata, in Greak, maana yake ni Zawadi, 1967 Dukwen University, 1993 ICCRS was instituted
1985 office za Karismaki zilianzishwa

Malengo:
NB Malengo ya Kanisa, ndiyo malengo ya Kanisa Katoliki Luk4:19-19 au Mathayo 28:18-20, Canon Law a210-2011.

1.Kusaidia watu wakue na kuendelea katika mahusiano binafsi na Utatu Mtakatifu: To Encounter with the person of Jesus Christ in your life.

2.Kuwasaidia watu wajue umuhimu wa Roho mtakatifu katika kuwaongoza, Kujue uwezo na kuonja nguvu za Roho mtakatifu

3.Kuwasaidia watu wapokee na kutumia karama za Roho mtakatifu latika kukijenga kanisa

4. Kufanya uinjilishaji kwa nguvu za Roho Mtakatifu. "Twendeni masokoni tuwahubirie, masokoni, mashambani, na kila mahali tuwahubirie watu wote habari njema" Rom10:17
Kuinjilisha walioko ndani ya kanisa, mifumo ya kijamii,

5. Kumshuhudia Yesu kwa maneno na kwa matendo.

6. Kusaidia watu kukua katika utakatifu, utume, ushiriki wa Sakramenti za kanisa, na kudumisha umoja wa kanisa kwa kuhimiza yale yafundishwayo na kanisa. Kuleta uhai katika liturjua

By Ev. Ladislaus T. Mulokozi

Copyright @ 2013 IFM CCR. Template by: Templateism